ILULA YETU

ILULA YETU
HOME: ILULA YETU BLOG

Alhamisi, 4 Januari 2018

Maelekezo ya Bodi ya Mikopo kwa wadaiwa ambao bado hawajaajiriwa


Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imewataka wanufaika wote wa mikopo ambao wanadaiwa na hawajaajiriwa bado, wafike katika ofisi za bodi hiyo zilizoko katika maeneo mbalimbali nchini ama kuwasiliana nao, ili wapewe maelekezo na utaratibu maalum wa namna ya kulipa mikopo yao.

Akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za Bodi ya Mikopo zilizoko Mwenge, Jijini Dar es Salaam, mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa elimu ya Juu (HESLB), Abdul-Razaq Badru ametoa wito kwa wale ambao bado hawajaanza kurejesha mikopo yao, hata kama bado hawajapata ajira maalumu, wafike katika ofisi za bodi maeneo mbalimbali nchini ili kupewa maelekezo na utaratibu wa namna ya kuanza kurejesja mikopo hiyo.

“Tunatoa wito kwa wale ambao kwa sababu fulani fulani walikuwa hawajaanza kulipa, walipe na wanakaribishwa kwenye ofisi zetu. Hata wale ambao hawako kwenye ajira maalum kuna utaratibu maalum tumewatengenezea. Wanaweza kuwasiliana na sisi katika mawasiliano yetu au wakaja ktika ofisi za Dar es Salaam, Dodoma, Mwanza, Arusha, Zanzibar na kwingineko il tuwape maelekezo na utaratibu maalum wa kulipa.” amesema Mkurugenzi Badru

Aidha Mkurugenzi Badru amesisitiza kuwa Bodi itahakikisha kuwa inawashughulikia wale wote ambao bado hawajarejesha mikopo yao ili waweze kuirejesha ikiwemo kuwachukulia hatua za kisheria na kuwafikisha mahakamani.

“Mtu yeyote aliyekopa mkopo kwa ajili ya kusoma, njia pekee ya kisheria inayoweza kumfanya asilipe mkopo huu, ni labda awe amefariki. Lakini kama umekopa, uko hai, uko hapa nchini na hata ukienda nje, sisi ni lazima utalipa huo mkopo kwa gharama yoyote ile,” amesisitiza.

Kwa upande wake Mkurugenzi Msaidizi Urejeshaji wa Mikopo, Phidelis Joseph amewataka wale ambao tayari wameshaanza kurejesha madeni katika akaunti za benki za Bodi ya Mikopo, waweke maelezo yote katika ”pay-in-slip’ zao.

“Wale wanufaika ambao wanajitokeza na wanalipa kwenye zile ‘bank accounts’ zetu waweke ‘details’ zote. ‘Unapodeposit’ unatakiwa utoe taarifa kwa Bodi ya Mikopo kwamba nimeweka pesa. Lakini vie vile unapoiandika ile ‘slip’ yako uiandike vizuri..,” amesema Phidelis Joseph.

Vile vile amewataka wanufaika wa mikopo ambao wameshaanza kulipa, wafike katika ofisi za Bodi ya mikopo ama kutumia mitandao ya Bodi, kwaajili ya uhakiki.

Jumamosi, 10 Juni 2017

Meya wa Jiji la Arusha Amtaka Mkuu wa Mkoa Amuombe Radhi

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiOmEdbmM8osV5X4ENwwYaQm69EhDdVj1Qxz1Y4ySgiUtrXlu1OCMatjTj6t-wIcCu7M6wPcy8KxwsiB2gLFcWuwLvG9qThyphenhyphenWurT6CHdzHwK6EGgAKAHwfDBWvC6yJ8m5YKiZu5G0IEieOX/s1600/1.JPGMeya wa Jiji la Arusha, Calist Lazaro ametoa siku saba kwa  Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo amuombe radhi kwa kosa la kumuweka ndani wakati alipokuwa anakabidhi rambirambi kwa wazazi waliofiwa kwenye ajali ya gari la Shule ya Msingi Lucky Vincent.

Akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake jana Ijumaa, Lazaro alisema mpaka sasa ameshindwa kuelewa ni kwanini mkuu huyo aliagiza meya pamoja na wenzake wakiwemo viongozi wa dini, madiwani, wawakilishi waliotoa rambirambi na mwenye shule kukamatwa na Jeshi la Polisi na kuwekwa ndani.

"Mimi sikuwa na shida na RC na kitendo cha kumuweka ndani kiongozi wa dini, paroko, kiongozi wa dini ya Kiislamu ni kitendo ambacho si cha kibinadamu na anapaswa aombe radhi umma,"alisema.

Pia, alimtaka kutafakari nafasi yake na kuona kuwa anafaa kuendelea kuwa mkuu wa Mkoa wa Arusha kwasababu ameonyesha kuwatumikia wananchi ambao hawaheshimu.

"Hana heshima na mbunge, madiwani, watu wenye degree zao, haheshimu viongozi wa dini halafu bado anataka uongozi,"alisema.

Jumamosi, 6 Mei 2017

Yanga, Prisons kumekucha

View CommentsMABINGWA watetezi wa Ligi Kuu Soka Tanzania Bara, Yanga leo wanashuka dimbani kuivaa Tanzania Prisons katika mchezo wa ligi hiyo kusaka pointi tatu muhimu kuelekea kwenye harakati zao za kutetea taji hilo.
Mchezo huo utachezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Yanga imetoka kupoteza mchezo wake wa nusu fainali Kombe la Shirikisho la Azam kwa kutolewa na Mbao FC baada ya kufungwa bao 1-0.
Huenda ikautumia mchezo huo kutafuta ushindi na kupoza machungu ya mashabiki wake baada ya kushindwa kusonga mbele hatua ya fainali ya michuano ya shirikisho. Katika mchezo wa raundi ya kwanza, Yanga ilishinda kwenye Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya bao 1-0.
Pia, katika mchezo wa robo fainali FA, Yanga iliwafunga tena Prisons mabao 3-0. Mchezo wa leo hautakuwa rahisi kwa pande zote Yanga ambaye anataka kupata pointi zitakazomsaidia kukimbizana na Simba kileleni kwenye msimamo, lakini pia, Tanzania Prisons ambao wana pointi 31 zisizotosha kuihakikishia kubaki salama.
Yanga yenye pointi 56 iwapo itashinda itafikisha 59 na kubakiza michezo minne mkononi, lakini kuna nafasi kubwa ya kupanda kileleni akiongoza kwa magoli mengi ya kufunga lakini iwapo Simba yenye pointi sawa na hizo 59 itashinda kesho dhidi ya African Lyon, basi Yanga itashuka nafasi ya pili.
Kocha Msaidizi wa Yanga, Juma Mwambusi alisema wachezaji wote wanaendelea vizuri na wapo tayari kwa mchezo huo. “Tunashukuru Mungu wachezaji wote waliokuwa Mwanza wanaendelea vizuri, tumejipanga kuhakikisha tunapata ushindi,”alisema.
Aidha, Azam FC inayoshika nafasi ya tatu kwa pointi 46 itawakaribisha Mbao FC kwenye uwanja wa Azam Complex, Chamazi. Timu zote hizo hazina inachogombea zaidi ya kutafuta ushindi wa heshima.
Lakini zaidi Mbao FC yenye pointi 30 inahitaji ushindi kujiondoa katika hatari ya kushuka daraja. Kwani nafasi iliyopo ya 12 ni hatari kwake kutokana na kufanana na timu nyingine na kwa tofauti ndogo ya pointi hivyo, akifungwa na wengine wakishinda atakuwa hatarini zaidi.
Ruvu Shooting yenye pointi 32 itacheza na Kagera Sugar yenye pointi 46 zaidi anayetakiwa kupambana na kushinda ni Ruvu. Hata Kagera kama inataka kuendelea kumaliza ligi katika nafasi tatu za juu anahitaji kushinda.
Michezo mingine itakayochezwa leo ni Toto African yenye pointi 26 dhidi ya JKT ruvu yenye pointi 23. Huu pia huenda ukawa ni mchezo mgumu kwa kila mmoja kutokana na kwamba wote wanashikilia mkia wakiwa hatarini kushuka daraja. Majimaji yenye pointi 26 inatarajia kucheza na Mwadui yenye pointi 35.
Mchezo huo ni muhimu kwa Majimaji kushinda na kujiondoa kwenye hatari ya kushuka daraja.

Jumatano, 8 Machi 2017

Rais Magufuli na mkewe wawasili mkoani Dodoma

Rais wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, amewasili Mkoani Dodoma ambako pamoja na mambo mengine ataongoza Kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa, Mkutano wa Halmashauri Kuu ya Taifa na Mkutano Mkuu Maalum wa Chama Cha Mapinduzi.

Mhe. Dkt. Magufuli ambaye ni Mwenyekiti wa CCM ataongoza kikao na mikutano hiyo kuanzia tarehe 10 - 12 Machi, 2017 Mjini Dodoma.

Mhe. Rais Magufuli akiwa na Mkewe Mama Janeth Magufuli waliwasili jana katika Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma akitokea Mkoani Morogoro ambako jana tarehe 06 Machi, 2017 alizindua uwanja wa kisasa wa ndegevita wa Ngerengere.

SAA MBILI ZA MAANDAMANO WANAFUNZI BARIADI, Zilivyo simamisha mji wa Bariadi.

Wanafunzi wa shule ya sekondari Bariadi iliyoko katika halmashauri mjini wa Bariadi Mjini Bariadi wakiandamana katikati ya barabara kuu ya Bariadi-Lamadi, mjini Bariadi wakishinikizwa kurudishwa Mkuu wa shule yao ambaye alikuwa amepewa uhamisho Deus Toga, ambapo alikuwa amepelekwa shule ya sekondari Giriku na kuletewa Mkuu wa shule mwingine Paul Lutema ambaye walimkataa.